Rais wa Marekani Donald Trump amewasili nchini China
Rais wa Marekani Donald Trump amewasili nchini China kwa ziara ya siku mbili, ambapo atakutana na mwenyeji wake Rais Xi Jinping. Hii ni ziara ya kwanza China inayofanywa na Rais wa Marekani aliye madarakani tangu mwaka 2017. Mkutano kati ya viongozi wawili wenye nguvu zaidi duniani huenda ukawa mojawapo ya mikutano muhimu zaidi katika muda wa miaka mingi.
#Trump #China #Xi #Jinping #dontv